WATUMIAJI WA ‘KISIMBUZI’ CHA ZMUX PEMBA, WAFOKA UKOSEFU WA HUDUMA ZA UHAKIKA.

Hassan Msellem
0

Watumiaji wa KISIMBUZI cha Uunganishaji na Urushaji wa Maudhui Zanzibar ‘ZMUX’ katika kijiji cha Wambaa Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba, amelalamikia ukosefu wa huduma za uhakika kutoka kwa kampuni hiyo kwa kipindi cha muda mrefu, jambo ambali linapelekea kutokufikia malengo ya kununua Kisimbuzi hicho.


Wakizungumza na idawaonline.com baadhi ya wateja hao, wamesema tangu wanunue kisimbuzi hicho hawajawahi kupata huduma kwa uhakika kama walivyotarajia na pindi wanapowasiliana na wahusika wanakosa majibu ya uhakika.


“Sisi wengine tangu tuliponunua ving’amuzi hivi hatujawahi kucheka kwa maana ya kupata huduma za uhakika tunalipa kila mwezi lakini ukija kuwasha tv ni michenga tu hakuna kiacho onekana, kwahivyo tumeshachoka kama ZMUX wameshashindwa watuambiaje tutafute ving’amuzi vyengine mbona vipo vingi tu na viko vizuri lakini tuliona hii ni bidhaa ya nyumbani wacha tuunge mkono” alisema mmoja miongoni mwa wateja hao

 

“Ebwana sisi tuliamini kingamuzi cha ZMUX kitatusaidia katika masuala ya michezo hususan BACLAYS PREMIER LEAGUE ya pale Uingerza lakini matokeo yake kwamba King’muzi hichi sisi tunalipia na tukishamaliza kulipia hapo huoni tela lolote na tuliamua kuchukua king’muzi cha ZMUX hichi king’muzi ni king’muzi cha Zanzibar  na sisi Wazanzibari tunapenda vitu vyetu lakini matokeo yake imekuwa ni matapeli na tukiwatafuta wanatuzungusha tu” Haji Khamis Simba mteja ZMUX

 

Ili kupata ufafanuzi juu ya joto hilo linalowakabili wateja hao, idawaonline.com ilifanikiwa kuzungumza na mhandishi kutoka kampuni hiyo ndugu Yusuf Haji Juma, ambapo amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo ya kiufundi katika mnara wa kurushia matangazo wa Kichunjuu Pemba na kuahidi kufanyiwa matengenezo hivi karibuni.

 

“Kwanza tunaendelea kuwaomba radhi wateja wetu wote ambao bado wanakabiliana na changamoto ya ukosefu wa huduma zetu kupitia mnara wa KIchunjuu, kwasababu kwa kipindi sasa huduma kupitia mnara wetu wa Kichunjuu zilikuwa zinasitasita kutokana na hitilafu ya ambazo zimejitokeza na tulikuwa tunatoa taarifa kupitia vyombo mbali mbali mpaka kupitia televisheni ya taifa ‘ZBC’ mafundi wetu wa ndani walifanya juhudi kubwa sana kuhakikisha huduma zinarejea tena kwa wakati lakini kwa kuwa haya mambo ya kiufundi yanahitaji utaalamu sana tuka wasiliana na wenzetu kutoka Ujerumani waje watusaidie namna ya kuweza kutatua  changamoto hii ambayo imejitokeza katika mnara wetu wa Kichunjuu, hivyo hapa tunapozungumza tumeshapata ujio wa wenzetu kutoka Afrika ya Kusini kwasababu wele wenzetu wa Ujerumani wametuunganisha na ma agenti wao kutoka Afrika Kusini na tayari wamefika nchini kwa kuanza taratibu za kufika Pemba katika mnara wetu wa Kichunjuu kuja kutatua hilo tatizoa ambalo limejitokeza” Mhandisi ZMUX.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top