AUAWA NA RAFIKI YAKE KWA KUKATAA KULIPA DENI LA TSH ELFU MBILI (2000)

0

 Kijana mwenye umri wa miaka 22, Nasoro Almas Mkazi wa Mtaa wa Mgulu wa Ndege Manispaa ya Morogoro ameuawa kwa kuchomwa kisu shingoni na Rafiki yake aitwaye Frank (anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 25-30), chanzo kikiwa ni Nassoro kumdai Tsh.Elfu mbili Frank baada ya kumkopesha siku chache zilizopita.


@ayotv_ imefika nyumbani kwenye msiba na kuzungumza na Mama wa marehemu Vumilia Nassoro ambapo amesema siku ya tukio Nassoro na Frank walitoka kwenye sherehe ndipo wakaanza kudaiana fedha hiyo “Mwanangu alipomuomba Frank amrejeshee Elfu mbili yake alikataa na kuibua mzozo uliosababisha Frank kuchukua kisu kwenye pikipiki yake na kumchoma shingoni Nassoro”


Mwenyekiti wa Mtaa wa Mgulu wa Ndege, Veronika Michael ametbitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema Mtuhumiwa amekimbia yeye pamoja na Mke wake na anaendelea kutafutwa.
Chanzo Millardayo
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top