KATIBU WA KANISA AJIUA KISA MZOZO WA KIMAPENZI NA MKE WA MCHUNGAJI MASANJA.

Hassan Msellem
0

Mwisho wa wiki iliyopita kulikuwepo na uvumi wa sakata la kujitoa uhai kwa katibu wa kanisa la Fell Free Church la aliyekuwa Mchekeshaji na Mchungaji Masanja Mkandamizaji kutoka Nchini Tanzania.

 


Taarifa zilisema kuwa katibu huyo alijitoa uhai kutokana na kujuilikana kwa kashfa ya kutoka kimapenzi na mama wa kanisa ambaye ni mke wa wa Mchungaji Masanja Mkandamizaji.

 

Ujumbe mrefu uliovujishwa kutoka kwa marehemu kabla ya kifo chake unaeleza kwa mapana sababu za kujitoa uhai katika sakata ambalo sasa limejumuisha mambo mengi ikiwemo suala la kuchepuka na mama wa kanisa.

 

Barua hiyo ilionekana kumuandikia mwanamke mmoja ambaye bado haijabainika kama ni kweli ni mke wake Mchungaji Masanja.

 

“Asante kwa kunipenda kipindi chote hakika umenipa upendo ambao umeacha alama moyoni mwangu ambao kila nikijaribu kuifuta nimeshindwa sioni upendo wako wa mwanzo hivyo nimebaki kuumia moyoni” Sehemu ya barua

 

Mchungaji Masanja ambaye kila Jumapili huwa anahubiri katika kituo cha Wasafi fm Radio, hakuhudhuria katika kipindi hicho kutokana na suala hilo tata ambalo linazidi kuchemka haswa kwenye mitandao ya kijamii.

 

Kupitia ukurasa wa Instagram, Mchungaji Masanja alipakia video yenye picha ya pamoja na mke wake wakionekana katika mkao wa kuomba na kusujudu na kuachia ujumbe wenye utata ambao wengi waliuwambatanisha na sakata hilo la kujitoa uhai kwa katibu katika kanisa lake.

 

Baada ya watu zaidi ya laki mbili kufurika katika ukurasa wa huo Mchungaji Masanja, na kuachia maoni mbali mbali, Mchungaji Masanja Mkandamizaji aliifuta maudhui hayo lakini kuna baadhi ya wale waliobahatika kuinakili na ilikuwa na maneno yafuatayo

 

“Kila kazi ina gharama yake. Acha tulipe gharama ya tulichoitiwa. Nakupenda mpaka pumzi yangu ya mwisho mke wangu. Hili nalo litapita. Tuombeeni nasi tunaomba. Mtetezi wangu yu hai” Aliandika Mchungaji Masanja

 

Katika maneno haya, wengi walionekana kukisia kuwa Mchungaji huyo alikuwa anatia roho ya kiume kusimama na mke wake wakati wa kipindi hichi kigumu ambacho kimezua hisia tofauti za kumsaliti mume wake na mfanyakazi wa kanisa hilo.

 

Wengine walisema kuwa huenda katibu huyo alijiua sit u kutokana na mzozo wa kimapenzi bali pia kutokana na msongo wa akili.

 

Inashauriwa kuwa kama umepetwa na hali inayopelekea kupatwa na tatizo la msongo wa mawazo kwa kukwazwa na mambo mbali mbali washirikishe ndugu, marafiki, washauri nasaha, madaktari pamoja wanasaikolojia ili kupata ufafanuzi juu ya kile kinachokukwaza.

 

Kwa msaada wa ushauri nasaha piga nambari hizi bila ya maliupo 1199.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top