KESI YA TUHUMA ZA KUBAKA MWALIMU WA SKULI YA MSINGI MADUNGU, ASKARI MPELELEZI AKAMILISHA USHAHIDI.

Hassan Msellem
0

Katika muendelezo wa kusikiliza mashahidi kwa upande wa walalamikaji dhidi ya kesi ya tuhuma za kumbaka mwanafunzi wa darasa la tano mwenye umri wa miaka 11 inayomkabili mwalimu wa skulia ya msingi Madungu, shahidi wa nne ambaye ni shahidi wa mwisho, upande huo umekamilisha ushahidi wake baada ya askari mpelelezi kutoa ushahidi mbele ya mahakama hiyo.

Akitoa ushahidi mbele katika kiriri cha mahakama hiyo, shahidi huyo amesema kwa mujibu upelelezi uliofanywa na jeshi la Polisi umegundua kuwa daftari la mahudhurio la Skuli lilionesha kuwa siku ambayo mwalimu huyo anatuhumiwa kufanya kitendo cha kumbaka mwanafunzi huyo aliingia kazini.

 

“Mheshimiwa hakimu kwa mujibu wa upepelezi ambayo jeshi la Polisi uliufanya ni pamoja na kufika skuli ambayo anasomesha mshitakiwa na kupatiwa daftari la mahudhurio ambapo limeonesha kuwa siku ya tukio mshitakiwa iliingia kazini” Alisema

 

Aidha, mpelelezi huyo alisema kuwa upelelezi uliofanywa na jeshi la Polisi umebaini kuwa kutokana na mazingira darasa ambalo muathirika alidai kuwa mshitakiwa aliitumia darasa hilo kumfanyia vitendo vya ubakaji, mshitakiwa anaweza kulitumia darasa hilo kufanyia vitendo hivyo kutokana na mazingira ya faragha ya darasa hilo na skulini hapo.

 

“Upelelezi uliofanywa na Jeshi la Polisi umebaini kuwa kutokana na mazingira ya darasa ambalo muathirika alidai kuwa alikuwa mwalimu analitumia kumbaka, jeshi la Polisi limejiridhisha kuwa mazingira ya faragha ya darasa hilo pamoja na mazingira ya skuli yenyewe mshitakiwa anaweza kulitumia darasa hilo kufanya vitendo hivyo” Askari mpelelezi.

 

Kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa na askari mpelelezi mahakamani hapo hakimu wa mahakama hiyo Muumini Ali Juma, amesema ameridhishwa na ushahidi huo na kumuamuru mshitakiwa kurudi rumande hadi tarehe 12.10.2022 kwa ajili ya kutoa uamizi mdogo.

 

“Kutokana na ushahidi ambao ametolewa na shahidi mahakama imeridhishwa na ushahidi huo na mshitakiwa atarudi tena rumande hadi tarehe 12.10.2022 kwa ajili ya uamuzi mdogo wa shitaka hili” Alisema


Ilielezwa mahakamani hapo kuwa siku ya tarehe 12.08.2022 majira ya 11:30 za jioni huko katika Skuli ya Msingi Madungu, Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, mshitakiwa alimbaka mwanafunzi wa darasa la tano mwenye umri wa miaka 11, jambo ambalo ni kosa kisheria kwa mujibu wa kufungu cha sheria ya adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.


Ikumbukwe kuwa kesi hiyo ilianza kutajwa mahakamani hapo Agosti 05.2022.

 

 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top