MAMA AITELEKEZA FAMILIA KIKIWEMO KICHANGA CHA WIKI TATU KWA MITOKO YA SEHEMU ZA STAREHE ZANZIBAR.

Hassan Msellem
0

Mama mmoja aliyefahamika kwa jina la Rahma Thabit Hemedi mwenye umri wa miaka 20, mkaazi wa Muembe Makumbi Mjini Unguja, amekuwa na tabia ya kuitelekeza familia yake ya watoto wanne (4) ikiwemo mtoto wake mchanga wa wiki tatu, jambo ambalo limezusha taharuki kwa familia na majirani wa mama huyo.

 


Akizungumza na kinasa sauti cha Mawio mama mzazi wa mwanamke huyo, amesema kuwa kawaida humshauri mama wa watoto hao kurudi mapema kwenye shughuli zake ili aweze kuishughulikia familia yake, lakini mama huyo ameshindwa kuufanyia kazi ushauri huo.

 

“Mie humwambia kama mtoto unamuacha urudi mapema kama vile saa 9, saa 10 lakini tangu hapo zamani  anamuacha anakwenda kwenye pirika zake ambazo sizijui hua naambiwa tu anakwenda Intebe, anakwenda Messi, Madisco disco sasa harudi mapema na kipindi hichi cha katika kati ndio haruuuudi kitoto kianlia na chakumfanya hatuna” alisema mama wa mwanamke huyu

 

Kwa upande wa majirani wa mama huyo, wamesema inapofika saa 11 za jioni mama huyo huondoka na kurudi saa 11 za jioni ya siku ya pili na kumnyonyesha mtoto na kuondoka tena na baadhi ya siku nyengine anashindwa kurudi.

 

“Kitoto anakiacha kinalia kina wiki tatu kinapewa uji wa sembe binafsi yangu mimi natoka na kwenda  kumkosha mtoto kazi yake kwenda Intebe na huyu ni mtoto wake wanne” Alisema mmoja wa majirani hao

 

Nae, sheha wa shehia hiyo Zubeir Othman, amekiri kuwepo kwa suala hilo na kusema kitendo ni udhalilishaji wa watoto na kudai kuwa mama huyo amekuwa na tabia hiyo ya kuitelekeza familia yake na kwenda sehemu za starehe kwa muda mrefu.

 

“Huu naweza kusema kama ni udhalilishaji wa watoto na huyu mtoto kusema ukweli ni shida mama mtu anatembea na ujusi ukiangalia hii familia yote kusema ukweli imeoza” Sheha wa Shehia ya Muembe Makumbi

 

Juhudi za Mawio za kumpata mama mzazi wa watoto hao zimegonga mwamba kutokana kutokujuiliakana alipo mama huy.

Chanzo. Kipindi cha Mawio

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top