MWAKILISHI WA JIMBO LA CHAMBANI ASAIDIA VIFAA VYA UJENZI TAWI LA CCM DODO PUJINI.

Hassan Msellem
0

Wanachama cha Mapinduzi ‘CCM’ tawi la Pujini Dodo wametakiwa kujitolea katika kuunga mkono juhudi za ujenzi wa tawi hilo ili ujenzi huo uweze kukamilika kwa wakati.


Kauli hiyo imetolewa na Mwakilishi wa jimbo la Chambani Mheshimiwa Bahati Khamis Kombo, wakati akikabidhi msaada huo wa mabati, boriti pamoja na makenchi huko katika tawi la CCM Pujini Kichanjaani, amesema viongozi wa CCM wa jimbo hilo la Chambani wanadhamira ya dhati ya kujenga na kuboresha matawi ya CCM, hivyo basi amewaomba wanachama wa tawi hilo kuunga mkono juhudi za ujenzi wa tawi hilo liweze kukamilika ujenzi wake kwa wakati.

 

“Sisi viongozi wenu tuna nia ya dhati katika kuhakikisha tunasaidia katika ujenzi wa matawi ya CCM katika jimbo letu la Chambani pamoja na kuyaboresha, kwahivyo niwaombe na nyinyi kuwa nia kama hiyo ili kuunga mkono juhudi hizi hususan nyinyi vijana kwasasabu nyinyi ndio nguvu kazi ya chama chetu na niwaombe muachane na propanga kuwa kujitoa katika ujenzi wa chama ni kupoteza muda” Mhe. Bahati Khamis Kombo

Mheshimiwa Mwakilishi wa Jimbo la Chambani Bahati Khamis Kombo, akizungumza na wanachama wa CCM tawi la Dodo Pujini baada ya kukabidhi msaada huo.


Kwa upande wake, Mbunge wa jimbo la Chambani Mheshimiwa Mohammed Abrahman Mwinyi, amewasihi wanachama wa tawi la Dodo Pujini kuthamini msaada huo uliotolewa na mwakilishi ili kuwatia moyo viongozi wa jimbo hilo.

Mbunge wa Jimbo la Chambani Mheshimiwa Mohammed Abrahman Mwinyi, akiwasihi wanachama wa tawi katika kujitolea kuunga mkono juhudi za maendeleo zinazofanywa na viongozi wa Jimbo hilo.


Nae, Mwenye kiti wa CCM jimbo la Chambani Ndugu Shaibu Ali Juma, amesema kutolewa kwa msaada huo ni miongoni mwa ahadi za viongozi wa jimbo hilo wakati wanaomba ridhaa ya kuchaguliwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 na hatimae kutimiza ahadi hizo kwa vitendo, jambo ambalo linatia moyo na kujenga imani kwa wanachama wa jimbo hilo.

Mwenye kiti wa CCM jimbo la Chambani Ndugu Shaibu Ali Juma.


“Viongozi wetu hawa ni viongozi wa mfano sana kwani walituahidi kutufanyia haya wanayotufanyia leo tangu wanaomba ridhaa kwenu, na hatimae tunashuhudia leo hii wanatekeleza kwa vitendo kwahivyo ni waombe tu ndugu wana CCM kuwaunga mkono pamoja kuungta mkono juhudi hizi” Alisema


Othman Hassan Omar, ni Katibu wa Siasa na Uenezi Wadi ya Dodo, kwa niaba ya wanachama na Uongozi wa Tawi hilo amewashukuru viongozi wa jimbo hilo akiwemo mbunge na mwakilishi kwa kujitoa kwao katika kuwasaidia wanachama wa jimbo hilo hususan katika ujenzi wa matawi pamoja sekta ya elimu.

Othman Hassan Omar, ni Katibu wa Siasa na Uenezi Wadi ya Dodo, akizungumza Kwa niaba ya wanachama wa tawi hilo baada ya kukabidhiwa msaada huo.


“Kwakweli tunajisikia furaha kweli kweli nah ii ni faraja kwetu kwasababu ni kilikuwa ni kilio chetu cha muda mrefu, lakini tuwashukuru viongozi wetu hawa wa jimbo letu kwa kujitoa kwa moyo wa dhati katika ujenzi wa matawi mbali mbali pomoja na sekta ya elimu katika jimbo hili kwakweli ni viongozi wa kuigwa” Katibu siasa na uenezi Wadi ya Dodo

 

Msaada huo umetolewa na mwakilishi wa jimbo la Chambani Mheshimiwa Bahati Khamis Kombo, ambapo umejumuisha korija saba za boriti na makenchi, mabati pamoja na misumari, ambapo vimegharimu shilingi milioni tano pamoja na fedha za ujenzi.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top