MWALIMU WA SKULI YA MSINGI MADUNGU ANAYETUHUMIWA KUMBAKA MWANAFUNZI WAKE AKUTWA NA KESI YA KUJIBU.

Hassan Msellem
0

Mahakama maalumu ya makosa ya udhalilishaji Mkoa wa Kusini Pemba Chake Chake, imesema mwalimu wa skuli ya Madungu msingi Ali Makme Khatib 25, anayetuhumiwa kumbaka mwanafunzi wake mwenye umri wa miaka 11 anayesoma darasa la nne, anakabiliwa na kesi ya kujibu juu ya shitaka hilo.


Hakimu wa mahakama hiyo, Muumini Ali Juma, alisema kinachoendelea juu ya mshitakiwa huyo, ni kujitayarisha kwa ajili ya kujitetea, hasa baada ya upande wa mashtaka, kufunga ushahidi wake.

 

Hakimu Muumini, aliyasema hayo Octoba 12.2022 mwaka huu wakati mtuhumiwa huyo anayewakilishwa na mawakili wawili dhidi ya shitaka hilo la kumbaka msichana wa miaka 11.

 

Hakimu huyo, aliuuliza upande wa utetezi juu ya njia watakayotumia kufanya utetezi, ikiwa ni ya kiapo, ambapo ukaeleza utatumia njia ya kiapo siku hiyo.

 

“Upande wa mashtaka tangu Octoba 11, mwaka huu ulishafunga ushahidi wake, baada ya kumsikiliza shahidi wake wa mwisho ambaye ni askari mpelelezi, hivyo mahakama imeona mshitakiwa anayo kesi ya kujibu” alisema hakimu Muumini

 

Wakili wa mshitakiwa Suleiman Omar Suleiman, alidai kuwa wako tayari kwa ajili ya kujitetea, juu ya tuhuma zinazowakabili mteja wao, kwa njia ya kiapo.

 

“Mheshimiwa hakimu tumeshauriana sisi mahakimu na mteja wetu kuwa, siku ya utetezi tutajitetea kwa njia ya kiapo na tunao mashahidi wetu wanne” alisema

 

Hivyo basi, baada ya pande zote mbili kukubaliana, mahakama imeghairisha shauri hilo hadi Octoba 17, mwaka huu, huku upande wa utetezi ukitakiwa kuwasilisha mashahidi wao.

 

Ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka Ali Amour Makame, alidai hana pingamizi yoyote na uamuzi huo wa mahakama, juu ya kujitetea kwa mshitakiwa huyo.

 

Awali ilidaiwa mahakamani hapo kuwa siku ya tarehe 12.08.2022 majira ya 11:30 za jioni huko katika Skuli ya Msingi Madungu, Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, mshitakiwa alimbaka mwanafunzi wa darasa la tano mwenye umri wa miaka 11, jambo ambalo ni kosa kisheria kwa mujibu wa kufungu cha sheria ya adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.

 

 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top