MWENYEJI WA MANYARA AJINYONGA ZANZIBAR, AACHA UJUMBE KWA FAMILIA “TUTAKUTANA MBINGUNI MUNGU AKIPENDA”

Hassan Msellem
0

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Samwel Edrew John mwenye umri wa miaka 31, mkaazi wa Welezo Unguja, ambaye ni mwenyeji wa Mkoa wa Manyara Tanzania bara, aliyekuja Zanzibar kutafuta maisha, amefariki dunia baada ya kudaiwa kujinyonga kwa kutumia kamba ya nailoni.

 


Tukio hilo, limebainika usiku wa Octoba 19 mwaka 2022 majira ya saa 4 za usiku huko Welezo.

 

Mawio imezungumza na rafiki wa marehemu huyo aliyegundua tukio hilo, amesema wakati akiwa anatoka kazini majira ya saa 4:50 za usiku amekuta mlango umefungwa na baada ya kusukuma mlango na kufanikiwa kuingia ndani ndipo alipokuta mwili wa marehemu ukiwa unaning’inia.

 

“Mimi hua nalala shamba kazini Chwaka lakini leo nimerudi usiku wa saa 4 kama na dakika hamsini nimekuta malngo umefungwa nikasukuma mlango ule msumari ukafunguka kuingia ndani nikamkuta mtu kanyooka kwenye dirisha kama kajinyonga nikatoka nje nikamuamsha mpangaji mwenzangu mmoja nikamueleza tukaenda kwa sheha na taratibu zingine zikafata” Alisema rafiki wa Samwel

 

Akithibisha kutokea kwa tukio hilo kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Elisante Makiko, amesema marehemu amekutwa amejinyonga chumbani kwa rafiki yake anayefahamika kwa Selevesta Donald Ako.

 

Aidha kamanda Elisante, amesema tukio hilo la kijana huyo kujinyonga limetokana msongo wa mawazo.

 

“Mtu mmoja ajuilikanae kama Samwel Endrew John amekutwa amejinyonga kwa kutumia kamba ya nailoni chumbani kwa rafiki yake aitwaye Selevesta Donald Ako, tukio hili la kijana kujinyonga inavyoonyesha ni kutokana na Msongo wa mawazo, ameacha ujumbe kwamba watu wampeleke ujumbe kwa mke wake kwamba ameamua kujinyonga lakini awatunze sana watoto Mungu akipenda wataonana na familia mbinguni kwa Baba” Alisema Kamanda Elisante

 

Mwanaidi Ali Daudi, ni Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano hospitali ya rufaa Mnazi Mmoja, amesema mnamo majira ya saa 9 za usiku askari wa Mwera waliufikisha mwili wa marehemu hospitalini hapo na uchunguzi uliyofanyika haukugundua jeraha lolote katika mwili wa marehemu.

 

Aidha, amesema mwili wa marehemu huyo ulikuwa unatoa harufu inayodhaniwa kuwa alitekeleza kitendo hicho cha kujinyonga siku moja kabla na tayari mwili wake umeshachukuliwa na ndugu zake kwa ajili ya kuanza taratibu za mazishi.

 

Chanzo. Kipindi cha Mawio.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top