SERIKALI YASEMA ZURU NYATO ATAKATWA MSHAHARA WAKE MIAKA 3,KISA MKASA HIKI HAPA

0

 

Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe mkoani humo imeagiza kukatwa mshahara asilimia 15 kila mwezi kwa muda wa miaka mitatu, Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Masage, Kata ya Kidugala, Zuru Nyato baada ya kubainika kughushi nyaraka za serikali na kusababisha hasara.

Akizungumza baada ya kikao cha uamuzi wa baraza,  Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Agnetha Mpangile alisema kosa hilo ni kinyume cha kanuni 42 Jedwali la 1 sehemu A(1) ya Kanuni ya Utumishi wa Umma ya Mwaka 2003, ikisomwa pamoja na kanuni D.12 na Kanuni  F27(1)(a) ya Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma toleo la mwaka 2009.

Mpangile alisema, watumishi wengine watatu waliokuwa na masuala ya kinidhamu, baraza limeagiza wapewe adhabu ya karipio kali la maandishi.

Alisema watumishi wanapaswa kuwa na maadili ya kazi na kufuata mwongozo na nidhamu pamoja na taratibu za kiutumishi.

“Kufanya udanganyifu kwenye mambo ya fedha sio uadilifu na wala sio utumishi, hivyo ninawaasa watumishi wote, hawa ni mfano lakini kama kuna tabia ambazo zipo katikati ya watumishi wetu, basi wanatakiwa waache mara moja na kufanya kazi kwa uadilifu, vinginevyo hawa tungewachukulia hatua kubwa. Kwanza wamemdanganya mwajiri wao na halmashauri," alionya.


Diwani wa Itulaumba, Thobias Mkane alisema watumishi wa umma wanapaswa kushirikiana kulinda fedha za serikali na michango  ili kuleta tija kwa wananchi Inaelezwa kuwa nyaraka zilizoghushiwa ni za michango ya wananchi kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya kijiji baada ya mtendaji huyo kutakiwa kurejesha kwenye akaunti fedha hizo.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top