DIRECT AID, KWA KUSHIRIKIANA NA TAASISI YA FARAJA YETU, YATOA MSAADA WA NG’OMBE KWA WAJANE WENYE WATOTO YATIMA, PEMBA.

Hassan Msellem
0

Shirika la Direct Aid kwa kushirikiana na taasisi ya Faraja Yetu Kisiwani Pemba, limetoa Ng’ombe wanne kwa familia mbili za wajane wenye watoto yatima ili kuwasaidia kutokana na hali ngumu ya maisha inayowakabili.

 


Akikabidhi msaada wa Ng’ombe hao, Mkurugenzi kutoka Shirika la Direct Aid Pemba Mohammed Elsayed, amesema Shirika hilo limeamua kutoa msaada huo wa Ng’ombe kwa watu wanaoishi katika mazingira magumu ikiwemo wajane na mayatima ili kuwapa nyenzo zitakazowasaidia katika kukabiliana na maisha.

 

“Today is a day of comfort for these families and for the leadership of Direct Aid and Faraja Yetu institution for our families who live in difficult circumstances, we believe that this support will be a good opportunity to develop yourself in life inshallah” Mkurugenzi Direct Aid


Kushoto ni Mkurugenzi wa Shirika la Direct Aid Mohammed El Sayed, akisikiliza Neno la shukurani kutoka Kwa katibu wa taasisi ya Faraja Yetu, Ali Juma Ali katikati.


Kwa upande wake Katibu wa taasisi ya Faraja Yetu Ndugu Ali Juma Ali, amelipongeza Shirika hilo kwa kushirikiana na taasisi ya Faraja Yetu katika kuwasaidia wananchi wanaoishi katika mazingira magumu ikiwemo wajane, watoto yatima pamoja na watu wenye ulemavu.

 

Mariam Juma Mcha, mkaazi wa Shehia ya Chole Mwambe ni miongoni mwa wanafamilia waliopatiwa msaada huo, amelishukuru Shirika la Direct Aid kwa kuwapatia msaada huo wa Ng’ombe wawili na kuahidi kuwatunza ili waweze kuwa nyenzo ya maendeleo katika maisha yake.

 

Mariam Juma Mcha, Mkaazi wa Chale Mwambe akisaini hati ya kukabidhiwa msaada huo.


Nae Bi. Mayassa Mohammed Hassan, mkaazi wa Chokocho, ameliomba shirika hilo kwa kushirikiana na taasisi ya Faraja Yetu kuendelea kuwasaidia watu wanaoishi katika mazingira magumu ili nao waweze kuishi kwa furaha na amani.


“Kwakweli tunashukuru sana sana kwa kutupatia msaada huu na tunatumai kuwa hali zetu zitaweza kuimarika hapo baadae, ila ombi langu kwenu muendelee kuwasaidia watu wenye hali ngumu ili nao waishi kwa furaha na amani” Alisema


Mkurugenzi wa Shirika la Direct Aid Pemba Mohammed El Sayed, akisaini mkataba wa msaada huo.

Lengo la msaada huo ni kuwawezesha kiuchumi watu wanaoishi katika mazingira magumu ikiwemo wajane, watoto yatima na watu wenye ulemavu Kisiwani Pemba.

Msaada huo wa Ng’ombe wanne kwa familia mbili zenye watoto yatima, umetolewa na Shirika la Direct Aid kutoka Nchini Kuweit kwa kushirikiana na taasisi ya Faraja Yetu kutoka Wilaya ya Mkoani Pemba.


Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top