VIONGOZI WA CCM WALIOCHAGULIWA NGAZI YA WILAYA WAHIMIZWA KUSIMAMIA MISINGI YA UMOJA NA MSHIKAMANO.

Hassan Msellem
0

Wito huo umetolewa na mjumbe wa kamati kuu ya halmashauri kuu ya CCM Taifa Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla, aliokuwa akizungumza katika mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa CCM Wilaya ya Domani Kichama.



Mheshimiwa Hemed, ambaye ni Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar, amewahimiza wajumbe kuchagua viongozi ambao watakivusha Chama kwenye katika uchaguzi Mkuu wa Dola mwaka 2025.


Aidha amewataka wanachama kuacha majungu na fitna na makundi yasiyokuwa na tija Kwa mustakbali wa Chama sambamba na kuwataka kutoa ushirikiano Kwa viongozi wapya katika kujenga Chama imara.

Baadhi ya wajumbe walioshiriki katika uchaguzi wa CCM ngazi ya Wilaya.

Nafasi zilizogombewa katika uchaguzi huo, ni ya Mwenyekiti wa CCM Wilaya, katibu wa siasa na uenezi wa Wilaya, wajumbe kumi wa halmashauri kuu ya Wilaya, wajumbe wawili wa mkutano mkuu wa Mkoa na wajumbe watatu wa mkutano mkuu Taifa.

Katibu wa CCM Wilaya ya Mkoani, Nicholas Samson Chibwana, akitaja orodha ya majina ya wagombea wa nafasi wajumbe kumi wa halmashauri kuu Wilaya. 

Wa kwanza kulia ni Mwakilishi wa Jimbo la Chambani Mheshimiwa Bahati Khamis Kombo, akifuatilia zoezi la upigaji kura katika Uchaguzi huo.
Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Mheshimiwa Khatib Juma Mjaja, ambaye ni mwangalizi wa Uchaguzi huo na Mjumbe.

Chanzo. ZBC RADIO

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top