Huko nchini Nigeria kundi la wanawake wanaotafuta waume wa kuwaoa hivi karibuni walitrend kwenye mitandao ya kijamii baada ya video moja kuchapishwa ikiwaonesha wanawake hao walivyoshiriki ibada ya maombi ya kuwapata wanaume wa kuwaoa katika kanisa moja huko nchini Nigeria.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kanisani hapo, Mchungaji kiongozi wa kanisa hilo aliwaagiza wanawake hao wanatafuta wanaume wa kuwaoa kuhudhuria ibada hiyo huku wakiwa wamevaa magauni ya harusi, wafanye maombi ya pamoja ili Mungu awawezeshe kupata wanaume watakaowaoa.
Wanawake hao walihudhuria na kushiriki ibada hiyo kanisa hapo wakiwa wamevalia magauni ya harusi huku wakiwaombea waume wanaowahitaji wawapate wakiamini kwamba baada ya maombi hayo, watakutana na wanaume wa ndoto zao na kuwaoa.
TAZAMA VIDEO HII