AFISA KILIMO AKAMATWA AKIOMBA RUSHWA YA TSH.10,000/=

0

 

Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Njombe imemkamata na kumfikisha Mahakamani Rashid Mkocha ambaye ni afisa kilimo wa kata ya Mlowa halmashauri ya mji wa Makambako mkoani Njombe kwa tuhuma za kumuomba rushwa ya shilingi elfu kumi (10,000) mkulima ili asajiliwe kwenye kitabu kwa ajili ya mbolea ya ruzuku.


Kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Njombe Kassim Ephrem amesema mtuhumiwa alikamatwa November 9 mwaka huu mara baada ya kupata taarifa kwa raia mwema na kuandaa mtego uliosaidia kumkamata mtuhumiwa.


“Tumemfungulia kesi afisa kilimo wa kata kwa kudai rushwa kwa mwananchi asajiliwe kwenye kitabu ili aweze kupata namba akachukue mbolea ya ruzuku halafu yeye ni afisa kilimo wa kata hata ukimuangalia mkulima unaona dah”amesema Kassim Ephrem.


Ametoa wito kwa kuacha vitendo hivyo kwa kuwa serikali ina nia njema ya kuwasaidia wananchi hivyo hawataweza kusita kumchukulia sheria mtumishi yeyote anayekwenda kinyume na sheria.

USIACHE KLUTAZAMA VIDEO HII 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top