DIWANI MWALYOYO AFARIKI DUNIA...DED MAKETE AMLILIA

0

 

Aliyekuwa diwani wa kata ya Kinyika wilayani Makete mkoani Njombe kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilbert Mwalyoyo amefariki dunia


Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Makete William Makufwe imesema kwamba diwani huyo amefariki dunia leo Novemba 16, 2022 wakati akipatiwa matibabu jijini Mbeya


"Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete kwa masikitiko makubwa anatangaza kifo cha Diwani wa Kata ya Kinyika  Mhe.Mwalyoyo kilichotokea leo tarehe 16.11.2022 jijini Mbeya.


Taratibu za mazishi zinafanywa na kwa mujibu wa wanafamilia  mazishi yatafanyika siku ya Ijumaa tarehe 18.11.2022 kijijini kwake Kinyika


Kwa niaba ya madiwani na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete natoa pole kwa familia, ndugu na jamaa wa Mhe. Mwalyoyo na kwamba Halmashauri inathamini na kutambua mchango wake katika  kuleta maendeleo kwa wananchi wa kata ya Kinyika na Halmashauri  kwa ujumla." 


Bwana alitoa, Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe.


William M.Makufwe 

Mkurugenzi  Makete DC.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top