KIJANA WA MIAKA 20, AHUKUMIWA KWENDA JELA AU KULIPA FAINI YA MILIONI 10, KWA KUJIFANYA RAIS SAMIA.

Hassan Msellem
0

Kijana Nickson Mfoi mwenye umri wa miaka 20, akitoka katika mahakama ya Hakimu Mkaazi Kisutu baada ya kuamuriwa kulipa faini ya shilingi milioni kumi (10) za Kitanzania au kutumikia kifungo cha miaka miwili jela baada ya kukiri kosa la kujifanya ni Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania SamIA Suluhu Hassan, kwenye mtandao wa facebook.

Na, Kamara Kenyunko, michuzi TV.


Shtaka jengine ni kuwa mshtakiwa alikutwa na hatimiliki na kutumia simu iliyo katika umiliki wa mtu mwengine bila ya kutoa taarifa kwa mtoa huduma.

 

Mfoi amekiri makosa yake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Richard Kabate baada ya kuomba kukumbushiwa mashtaka yake mahakamani hapo.

 

Kabla ya kusomewa adhabu yake baada ya kutiwa hatiani, upande wa mashtaka ukiongozwa na wakili wa Serikali, Ashura Mzava, ameiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshtakiwa ili iwe fundisho kwake na kwa wengine ambao wamekuwa wakiendelea na vitendo vya matumizi mabaya ya mitandao kwa kutumizi mabaya ya mtandao kwa kutumia majina ya viongozi na hata kuwakashifu.

 

Kwa upande wake mshtakiwa ameiomba mahakama imuonee huruma kwani wakati anatenda kosa hilo hakujua kama madhara yake ni makubwa.

 

Hakimu Kabate amesema, amepitia hoja za pande zote mbili na kuongeza kuwa “Ukimzungumzia    Rais na wazi kuwa umeizungumzia Tanzania nzima, personation iliyoko katika shtaka hili siyo ya kawaida na jina alilolitumia siyo la kawaida hivyo lazima uadhibiwe” Alisema Kabate

 

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Kabate amesema katika shtaka la kwanza la kujifanya yeye ni Rais Samia Suluhu Hassan smhtakiwa anapaswa kulipa faini ya shilingi milioni tano au kwenda jela mwaka mmoja huku pia katika shtaka la pili anapaswa kulipa shilingi milioni tani ama kutumikia kifungo cha mwaka mmoja gerezani.

 

Hata hivyo, mahakama imesema adhabu zote hizo zitakwenda pamoja ambapo mshtakiwa anapaswa kulipa shilingi milioni kumi na kama atashindwa basi atatakiwa kutumikia kifungo cha miaka miwili gerezani.

 

Katika hoja za awali inadaiwa mshtakiwa alitumia akaunti ya Facebook yenye jina la Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kwa kujiwasilisha kuwa yeye ni Rais Samia Suluhu Hassan.

 

Pia, mshitakiwa huyo alikiri kwamba kati ya Septemba, 2021 ndani ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa nia ya kulaghai uuma alijiwasilisha kama Rais Samia Suluhu Hassan kupitia akaunti yake ya Facebook.

 

Aidha, mshitakiwa huyo alikutwa na laini ya simu ambayo awali ilikuwa inamilikiwa na Getness Jackson kwa madai kwamba alipewa na mtu anayesajili laini.

 

“Ni kweli hii akaunti ya Facebook nilikuwa naitumia mimi, niluziwa lakini yaliyokuwa yakiendelea humo mimi siyajui na ni kweli nilikuwa natumia simu ambayo haijasajiliwa kwa kidole change” Alidai Mfoi

 

Mshtakiwa pia amekiri kwamba Septemba, 2021 alikamatwa na askari katika hoteli ya Malaika Mkoani Mwanza na alipopekuliwa alikutwa ana miliki simu moja na laini iliyosajiliwa kwa jina la Getness Jackoson bila ya kutoa taarifa kwa mtoa huduma, ambapo alikamatwa na Agosti 4, 2021 aliletwa mahakamani kwa ajili ya kujibu mashtaka yake.

 

 

 

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top