MAJAMBAZI WAVAMIA KANISA NA KUWAPORA WAUMINI

0

 Majambazi waliokuwa na silaha wamevamia kanisa huko Johannesburg nchini Afrika Kusini na kuwapora waumini huku wakiwatisha kwa bunduki, Jumamosi Novemba 26 mwaka huu.

PICHA KUTOKA MAKTABA HAIHUSIANI NA TUKIO HALISI

Kamera ya kanisa hilo iliwanasa majambazi hao ambao walisimamisha ibada na kuanza kukusanya pesa na vitu vya thamani kutoka kwa watu waliohudhuria ibada katika kanisa la SDA la Johannesburg Central,

Viongozi wa kanisa hilo baadaye walituma ujumbe wa kuwafariji waumini wao na kuwataka kuhudhuria ibada ya ushauri siku ya Jumapili, siku moja baada ya tukio hilo.

”Kanisa linapenda kuchukua nafasi hii kuwahakikishia kuwa hili nalo litapita. Hakuna kinachodumu milele. Kama viongozi, tunaombea kanisa kuungana katika nyakati kama hizi tukisaidiana kimaadili na kimatendo,” umesema ujumbe huo.

HIVI ULITAZAMA VIDEO HII? KAMA BADO HUJACHELEWA

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top