MUME ATUHUMIWA KUMUUA KWA KUMKATAKATA NA PANGA MKEWE SHAMBANI

0

Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro limatafuta Exavel Mgogo mkazi wa Manispaa ya Morogoro kwa tuhuma za kumuuwa mke wake Catherine Peter (27) kwa kumkata na panga sehemu mbalimbali za mwili wake.

PICHA KUTOKA MAKTABA
Mkuu wa upelelezi wa mkosa ya jinai mkoa Morogoro Raph Meela amesema tukio hilo limetokea novemba 21 2022 majira ya saa tatu asubuhi katika eneo la Star city kata ya Tungi.

Meela ameeleza kuwa mtuhumiwa huyo baada ya kutekeleza mauaji hayo alikimbia ambapo jeshi hilo linaendelea kumsaka.

Shuhuda wa tukio hilo ambaye ni dada wa marehemu Mary Peter amesema wakiwa shambani alifika Mume wa marehemu Exavel Mgogo ambaye ni mtuhumiwa na kufanya mazungumzo na mkewe ( marehemu) na mara baada ya kutoelewana alichukua panga alilokua ameficha na kuanza kumshambilia sehemu mbalimbali za mwili.

Mary amesema kuwa marehemu ameacha watoto watatu pia alikuwa mjamzito

Aidha Mary ameeleza kuwa wanandoa hao walikuwa na ugomvi wa mara kwa mara ndani ya familia.

KAMA HUJAWAHI KUTENGENEZA PESA MTANDAONI TUMIA NJIA HII SASA
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top