TAARIFA MPYA KUHUSU AJALI YA NDEGE NA AMBAO BADO HAWAJAOKOLEWA HII HAPA!

0

Watu watatu wamethibitishwa kufariki dunia katika ajali ya Ndege iliyotokea leo ziwa Victoria Mkoani Kagera ,watu 27 wakiokolewa na wengine 16 mpaka Saa kumi jioni taarifa zilizotolewa na mamlaka zimeeleza kuwa bado walikuwa wakiendelea kuokolewa kutoka kwenye Ndege hiyo.


Ndege ya  Precision Air ATR 42 yenye namba za usajili 5H BWF ilianguka majini ikitokea Dar es Salaam kuelekea Bukoba kupitia Mwanza leo asubuhi ikiwa na watu 43 (Wakubwa 38 na Mtoto mmoja) na Wafanyakazi wanne .

Baadhi ya mashuhuda walioshuhudia ajali hiyo akiwemo wamesema Ndege hiyo ilipoteza uelekeo kabla ya kutua uwanja wa Ndege.

INSERT;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;KAGERA 1

upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe Albert Chalamila amesema kutokana na ajali hiyo Waziri mkuu wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa anatarajiwa kufika mkoani Kagera ili kuungana na timu ya ukozi.



Mganga mkuu wa Mkoa wa Kagera Dkt. Issessanda Kaniki amethibitisha kupokea miili ya watu watatu waliofariki Dunia katika ajali ya Ndege iliyotokea mapema Asubuhi ya Leo.

Dkt. Kaniki amebainisha kuwa wamepokea watu 26 wakiwa Hai ambapo kati yao Wanaume 17, Wanawake 9, huku Wanaume 2 na Mwanamke 1 wakipokelewa wakiwa wamefariki dunia

Uongozi wa Shirika la Ndege la Precision Air kupitia Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo Patrick Mwanri umetoa taarifa kuhusu ajali ya Ndege yao iliyotokea Bukoba mkoani Kagera leo asubuhi wakati ikitua na kusema watashirikiana na familia za wahanga wa ajali hiyo kwa kila hatua.


Mwanri amewaomba waandishi wa habari kutoe taarifa sahihi ili kutopotosha umma kuhusu ajali hiyo kwani bado wanaendelea na uokozi wa watu wengine waliokwamba kwenye ndege.

Kwa upande wa Taarifa iliyotolewa na ENzalayaimisi Msemaji wa jeshi la Zima moto na uokoaji makao makuu Dodoma imesema kuwa mpaka majira ya saa kumi jioni Abiria 27 walikuwa wameokolewa,watatu wakipoteza maisha na juhudi za uokozi watu 16 waliokwama kwenye ndege zilikuwa zikiendelea

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameeleza kupokea kwa masikitiko taarifa ya ajali ya ndege ya Shirika la Precision katika Ziwa Victoria, mkoani Kagera.

Rais Samia ametuma salamu za pole kwa wote walioathirika na ajali hiyo huku akiwataka Watanzania kuendelea kuwa watulivu wakati huu zoezi la uokoaji likiendelea.

"Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya ajali ya ndege ya Shirika la Precision katika Ziwa Victoria, mkoani Kagera. Natuma salamu za pole kwa wote walioathirika na ajali hii. Tuendelee kuwa watulivu wakati huu zoezi la uokoaji likiendelea huku tukimuomba Mwenyezi Mungu atusaidie. - Rais Samia Suluhu Hassan


Precision Air ndiyo shirika kubwa la ndege la binafsi la Tanzania na kwa sehemu inamilikiwa na Kenya Airways. Ilianzishwa mnamo 1993 na inaendesha safari za ndege za ndani na kikanda.

Endelea kufuatilia mtandao huu tutakuletea taarifa mpya kila zinapotufikia,Mtandao huu unawaombea Dua njema waliolazwa wapone haraka na wanaondelea kuokolewa Mwenyezi Mungu! akawape pumzi ya subira kupata kuokolewa wakiwa hai. AMINA.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top