"Ni aibu kubwa shule moja siku moja ina watoro 500, imetokea katika wilaya hii na katika halmashauri hii", alisema Shimo"
Shimo ametoa maagizo hayo kwa walimu wakati anaongea na walimu, viongozi wa kata na wananchi kwenye mamlaka ya mji mdogo Katoro baada ya kuona utoro uliokithiri kwenye wilaya hiyo huku serikali imekuwa ikiboresha miundombinu ya elimu kila siku.
"Katika maeneo yangu imeonekana walimu wanafanya shughuli za bodaboda, walimu wengine wanauza maduka ya bodhaa mbalimbali na wengine wana kuwa na shughuli mbalimbali za namna hiyo, kuna wengine tumewakuta mwaka unakwisha form two kwa mfano wanafanya mitihani mwalimu hajamaliza topic tatu katika tisa sasa watoto wanaingia kwenye mtihani let say mtihani wa Physics, watoto wanaingia kwenye mtihani hawajamaliza topics tatu, sasa ujategemea watafanya nini? Moja kwa moja watafeli", alisema Manyonyi.
JE! UNAJUA UNAWEZA KUTENGENEZA KIPATO CHA ZIADA MTANDAONI? KAMA HUAMINI TAZAMA VIDEO HII.