WANAUME WADAI WANAWAKE WANAWAVIZIA WANAWAPIGA

0

Wananchi wa kijiji cha Ivalalila mamlaka ya mji mdogo wa Iwawa wilayani Makete Mkoani Njombe wamesema kuwa kwa sasa kipigo katika ndoa kimekuwa pande zote mbili bila kujali jinsia.


Wakizungumza katika mkutano wa hadhara katika kijiji hicho uliolenga kujengeana uelewa juu ya masuala ya ukatili kupitia mradi wa Mwanamke Imara chini ya WLDAF,wamesema kuwa baada ya kuendelea kutangazwa usawa wa kijinsia kumechangia wanawake kuwapiga wanaume.

Wanaume wanaaakili na wanawake wanaakili,unaweza ukajipanga leo umempiga si ndio,siku nyingine unajisahau anasema zamu yako leo unapigwa mwanaume’ amesema mmoja ya wanaume.

Baadhi ya wanawake katika mkutano huo wamesema kuwa wanaume wengi wamekuwa wakishindwa kutekeleza majukumu yao ikiwemo kuwajibika kutoa matunzo.

‘Unakuta mwanaume anachelewa kurudi nyumbani,anafika anataka chakula anakuuliza mbona hakuna nyama anataka wewe mwanamke ukatafute mboga nzuri’Amesema mmoja ya mwanamke.


Mwezeshaji Thomas Mponda kutoka Mradi wa Mwanamke Imara amesema vitendo vya ukatili havikubaliki na kuwataka wanaume kwa wanawake kuacha tabia ya kuwanyanyasa wenzao kulingana na jinsia zao.

‘Moja wapo ni ubakaji,kulazimishwa kufanya ngono lakini inaenda mbali sana hata kumshikaa mtu sehemu zake za siri bila ridhaa yake,hivyo vyote ni vitendo vya ukatili’ amesema Thomas

Kwa upande wake Wakili wa Mradi wa Mwanamke Imara Bi. Suzan Kiwanga amesema kumekuwa na mtazamo katika jamii kuwa Dawati la Jinsia ni kwa ajili ya wanawake na watoto pekee jambo ambalo sio sahihi na kuwataka wanaume nao kutumia dawati la Jinsia kuripotiwa vitendo vya ukatili wanapotendewa na wanawake.

Amesema Mwenendo wa maisha ya kila siku ya wanafamilia ndio matokeo ya familia ijayo ya watoto wao ikiwa baba atampiga mkewe basi mtoto hata yeye akiwa na familia ataona ni jambo la kawaida.


Amoni Mapunda kutoka Ofisi ya Ustawi wa Jamii Wilaya ya Makete amewasihi wananchi kuendelea kuwatumia maafisa Ustawi waliopo kuanzia ngazi za Kata na viongozi wa vijiji kuripoti matukio ya ukatili ili kuwepo na usawa wa kijinsia kwa watu wote.

Philipina Mkumbo Afisa upelelezi Wilaya ya Makete akizungumza kwenye Mkutano huo amesema, matukio ya ukatili yameendelea kuripotiwa katika Dawati la Jinsia Kituo cha Polisi Makete na vituo vidogo vya Polisi lakini wanaendelea kutoa elimu na ushauri namna ya kukabiliana na matukio hayo ya ukatili.

TAZAMA VIDEO HII ITAKUSAIDIA KUSAKA FURSA MTANDAONI

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top