Lakini jambo la kushangaza ni kwamba athari ya ukame zimewafanya wazazi kubuni njia za ajabu za kutoa matumaini kwa watoto wao.
Wazazi hao sasa wanapoesha makali ya njaa kwa kuwalazimisha watoto wao kutumia bangi na pombe ambayo ni ya bei nafuu na inayopatikana kwa urahisi katika kijiji hicho ili kuwazuia kuitisha chakula ambacho kwao ni dhahabu.
Kulingana na wazee wa kijiji hicho, wazazi hao hutumia chang’aa, bangi na dawa zingine za kulevya ambazo hupatikana kwa urahisi.
“Tunasikitishwa na ukweli kwamba baadhi ya wazazi sasa wanaamua kuwapa watoto bangi na vileo vya bei nafuu ili kusahau kula. Mara tu wanapotumia dawa mbalimbali zilizopigwa marufuku, watoto wengi huishia kulala,” Kimani alisema.
Wakaazi hao wanaokabiliwa na njaa waliiomba serikali kuchangia haraka chakula cha msaada katika eneo hilo ili kuokoa maisha.