BABA WA MIAKA (44) ALAZIMISHWA KUFANYA TOHARA

0
Mwanamue mwenye umri wa miaka 44, katika kaunti ya Bungoma nchini Kenya, alilazimishwa kukabiliana na kisu cha ngariba mbele ya mkewe na watoto wake watatu baada ya kukwepa kisu hicho kwa miaka kadhaa.

Peter Onyango, mkazi wa Lukhome katika kaunti ndogo ya Kiminini alipelekwa mtoni Jumamosi, Disemba 10,2022 asubuhi, na umati wenye ghadhabu, ambapo alipakwa matope kabla ya kuanikwa mbele ya watu kupashwa tohara.

Mkewe, Janet Musenya, alisema kwa muda wa miaka minane tangu walipooana, mumewe alikuwa akikwepa kisu cha ngariba na hivyo kumlazimu kupanga njama ya kutahirishwa kwake.

“Niligundua kuwa anaogopa maumivu lakini sikuweza kustahimili kuishi naye. Nina furaha kuwa sasa ni mwanaume kamili,” alisema.

Aliahidi kutekeleza majukumu yote ya kumuuguza mumewe hadi atakapopona kidonda cha kupashwa tohara. 

Kulingana na jirani wa wanandoa hao, Amos Sikuku alisema kuwa wanandoa hao walikuwa wanagombana na kwa hasira, mkewe Onyango aliropokwa na kuanika siri yao ya muda mrefu. Lakini Onyango alionekana kuwa na ahueni baada ya kukatwa, akisema alikuwa amekejeliwa kwa miaka mingi kwa sababu ya hali yake.

“Ninawaomba wasamaria wema kusaidia familia yangu kwa chakula katika wakati huuu ambao bado nitakuwa nikiuguza jeraha hili kwani siwezi kufanya kazi yoyote ya maana,” akasema baba huyo wa watoto watatu. 
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top