MFUNGWA AJIUA KWA SHUKA MKOANI MARA

0

 Thomasi Mwita Masiaga (28) mkazi wa Kijiji cha Itununu Wilaya ya Serengeti aliyekuwa anatumikia kifungo cha nje cha miezi 6 kwa kumfanyia kosa la kumpiga mke wake amekufa kwa kujinyonga siku aliyotakiwa mahakamani kwa kesi ya talaka.


Tukio hilo limeacha maswali mengi kwa ndugu zake kwa kuwa hakuacha ujumbe wowote licha ya kuwa alikuwa amewaandaa kaka yake na baba mdogo wake kwenda nao Jumatano Januari 18,2023 Mahakamani kwa ajili ya kutoa Ushahidi kwenye kesi ambayo mke wake anadai talaka.

Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Itununu kata ya Nyamoko Samwel Maitarya Jumatano Januari 18 amesema,Thomas amekutwa amekufa kwa kujinyonga kwa kutumia shuka kwenye mti wa Mkoma ulioko hapo kwao majira ya saa 11 alfajiri.

“Ni kweli huyu kijana amekufa kwa kujinyonga kwa kutumia shuka,hili jambo limetushangaza sana kwa kweli,tumetoa taarifa polisi ili waje kwa hatua zaidi za kiuchunguzi,”amesema.


Amesema,kwa mjibu wa maelezo ya mama yake amewaambia kuwa kutokana na kesi hiyo ya mke wake alikuwa anasema anaweza kujiua maneno ambayo wameamini baada ya kumkuta amekufa kwa kujinyonga.


Masanda Masiaga kaka wa marehemu Thomas ameiambia Serengeti Media Centre kuwa wameshangazwa na uamzi wa mdogo wake kujinyonga ”huyu tarehe 16 alipotoka Mahakamani alikuja na kunieleza mimi na baba mdogo  jumatano (18.1.2023) tukamtolee ushahidi wa kesi yake ambayo mke anadai talaka,”amesema.


Amesema,walikubali na walikuwa na maandalizi hayo,na baada ya hapo hakuwashirikisha chochote zaidi ya alfajiri kupigiwa simu kuwa kajinyonga,

kwanza alikuwa hajamaliza kifungo chake cha nje cha miezi sita alichofungwa kwa kosa la kumpiga mkewe,na kesi hii ambayo mke anaomba talaka ilikuwa inaelekea mwisho na yeye kaamua kajiua,”amesema.

Amekiri kwa muda mrefu kulikuwa na mgogoro baina yao wawili na kifamilia waliwahi kuwasuluhisha bila muafaka na kwa muda mrefu kidogo mke anaishi kwao na watoto,hata kwenye msiba hawajafika.

Kwa mjibu wa taarifa toka Mahakama ya Mwanzo Mugumu kesi hiyo ya Talaka imeahirishwa leo Januari 18 hadi 19,2023 baada ya mdai mke wake jina tunalo kufika na mdaiwa Thomas kutoonekana kwa kuwa hawakuwa na taarifa ya kujinyonga kwake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara Longinus Tibishubwamu alipotafutwa simu yake iliita bila kupokewa alipotumiwa maswali kwa njia ya ujumbe mfupi(Sms)licha ya kufika lakini hakujibu,hata hivyo Polisi wilayani hapa wamethibitisha na uchunguzi wa kitabibu umebaini chanzo cha kifo chake ni kukosa hewa kutokana na kujifunga na shuka shingoni na kutoa kibali cha mazishi.
BOFYA HAPA KUTAZAMA VIDEO HII
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)
Youtube Channel Image
Henrick Idawa Subscribe To watch How to Earn Money

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top