MTOTO ATUHUMIWA KUMUUA BABA YAKE KWA KUMCHOMA NA KISU.

0

Ni masikitiko. Hivyo ndivyo unavyoweza kusema baada ya mzee wa miaka 81, Dionis Lyimo, mkazi wa kijiji cha Nduweni, Kata ya Marangu Magharibi, Wilayani Moshi, mkoani Kilimanjaro kudaiwa kuuawa kikatili na mwanaye wa kumzaa saa chache kabla ya kuingia mwaka mpya 2023.


Inadaiwa mzee huyo kwa miaka mingi amekuwa akiishi maisha ya mateso na dhiki kubwa kutokana na manyanyaso, ikiwemo vipigo alivyokuwa akivipata kutoka kwa mtoto wake huyo, anayetambulika kwa jina la Prosper Lyimo (47).

Mzee huyo anadaiwa kupigwa mawe na kuchomwa na kisu cha kukatia majani ya ng’ombe (shami) kichwani, alifariki dunia usiku wa Desemba 31, 2022 nyumbani kwake baada ya kushambuliwa na mwanaye huyo aliyekimbia kusikojulikana baada ya tukio hilo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simoni Maigwa alithibitisha kutokea kwa mauaji hayo na wanamsaka mtuhumiwa huyo na atakapopatikana atafikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)
Youtube Channel Image
Henrick Idawa Subscribe To watch How to Earn Money

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top