MWANACHUO ALIYEPOTEA AKUTWA AMEFIA NYUMBANI KWA MPENZI WAKE.

0

 


Mwanafunzi wa kike katika Chuo Kikuu cha Kenyatta, aliyetoweka wikendi iliyopita, alipatikana amefariki katika nyumba ya mpenzi wake mtaa wa Kahawa Wendani, Kaunti ya Kiambu nchini Kenya.


Victoria Muthoni Theuri, mwanafunzi aliyekuwa akisomea Sera ya Umma na Utawala, alionekana mara ya mwisho Siku ya Krismasi mwaka jana.

USIPITWE NA VIDEO HII MUHIMU KWA MWAKA 2023

Siku hiyo, aliwaambia wazazi wake wanaoishi katika eneo jirani la Kahawa Sukari katika Kaunti ya Kiambu kwamba alikuwa anaenda kumtembelea dadaake.

Imeelezwa kuwa jioni ya siku hiyo baada ya mwanafunzi huyo kukawi kurejea nyumbani wazazi waliamua kumpigia dada yake simu kujua ikiwa atalala kwake lakini hata hivyo hakuwa amefika pia kwake.


Alipokosa kurudi nyumbani siku iliyofuata huku simu yake ikiwa bado imezima, wazazi wake waliripoti tukio hilo katika Kituo cha Polisi cha Kahawa Sukari.

Baada ya siku chache harufu iliyokuwa ikitoka katika chumba cha mpenzi wake kiliwashtua majira ambao baada ya kutoa taarifa na kufungua chumba hicho walikuta mwili wa mwanafunzi huyo.

“Mwanamume anayeishi hapo hakuwepo na tuligundua kuwa kulikuwa na harufu mbaya kutoka kwa nyumba. Ilinuka kama kitu kilichooza ndani ya nyumba iliyofungwa,” jirani alisema.

Jeshi la polisi katika Kaundi hiyo wameanzisha uchunguzi na kumsaka mpenzi wa msichana huyo ambaye alitokomea baada ya mkasa huo.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)
Youtube Channel Image
Henrick Idawa Subscribe To watch How to Earn Money

 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top