UMBALI WA UPATIKANAJI WA HUDUMA ZA KIPOLISI NA MAHAKAMA KWA WANANCHI WA KISIWA CHA MAKOONGWE, NI CHANZO CHA KUKOSA HAKI ZAO.

Hassan Msellem
0

Wananchi wa Kisiwa cha Makoongwe Mkoa wa Kusini Pemba, wameiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kuwasogezea kwa ukaribu huduma za kipolisi na mahakama ilikuepukana na usumbufu wanaokumbana nao wakati wakihitaji huduma hizo.

 


Wakizungumza kwenye mkutano maalum na watendaji wa mahakama huko skuli ya Makoongwe, wamesema umbali wa upatikanaji wa huduma hizo unachangia kwa kiasi kikubwa kutokupata haki zao kwa wakati sambamba na kukosekana kwa haki hizo.

 

Alieleza mmoja wa wananchi “Waheshimiwa chanzo kikubwa kwa sisi wananchi wa Makoongwe masafa makubwa ya upatikanaji wa huduma za Polisi na Mahakama, kama munavyofahamu kuwa sisi tuko kwenye Kisiwa na huku hakuna hata kituo kidogo cha Polisi kwahivyo mwananchi anapokuwa na kesi yake inambidi mpaka avuuke mpaka Mkoani ndipo apate kituo cha Polisi na kuanza mchakato wa kwenda mahakamani, kwahivyo tunawaomba sana kwa hili mutuangalie ili na sisi tuapate angalau kituo kidogo cha Polisi ili tuweze kupeleka kesi zetu”

 

“Binafsi nilikuwa na kesi ya mume wangu ya kunitelekeza na familia nilipambana sana ili kuhakikisha napata haki yangu lakini kutokana umbali wa huku ninakoishi gharama zinakuwa ni kumbwa mno na dana dana zilikuwa nyingi nikashindwa kuapata haki yangu hadi niliposafiri kwenda Unguja ndipo nikafanikiwa” alisema mama huyu

 

Alieleza changamoto mbali mbali walizoziibua mara baada ua kumalizika kwa mkutano huo, Naibu Mrajis wa mahakama Kisiwani Pemba Faraji Shomari Juma, amesema wamegundua uwepo kesi za familia ikiwemo utelekezaji wa familia, utoaji wa talaka kiholela pamoja na migogoro ya mirathi.

 

“Katika mkutano huu tumegundua changamoto mbali mbali zinazowakabili wananchi miongoni mwa changamoto hizi ni pamoja migogoro ya kifamilia ikiwemo talaka za mara kwa mara pamoja mirathi, na wananchi hawajui chakufanya ni nini pindi inapotokea hiyo migogoro lakini tunashukuru sana ujio wetu huu umeweza kutoa mwanga kwa wananchi hawa na ni matumaini yetu kuwa wataitumia elimu kwa kutoa taatifa kwa vyombo vya dola na sheria pindi wanapokumbwa na changamoto mbali mbali za Kisheria” Naibu Mrajis wa mahakama Pemba

 

Akitoa ufafanuzi juu ya changamoto zinazowakabili wananchi hao, kadhi wa rufaa Pemba Sheikh Daudi Khamis Salim, amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeweka utaratibu nzuri wa gharama nafuu za ufunguaji wa kesi ili wananchi waweze kupata haki zao kwa urahisi.

 

“Ukweli ni kwamba Serikali imeweka gharama nafuu sana za ufunguaji wa kesi katika mahakama ya kadhi ili wananchi waweze kuhimili kufungua kesi na kupata haki zao na niwaase wasiogope na wafike mahakama ya kadhi pindi wanakuwa na migogoro mbali mbali ya kifamilia pamoja na mirathi” Kadhi wa Rufaa Pemba 


Mkutano huo maalum baina ya wananchi wa Makoongwe na watendaji wa mahakama Kisiwani Pemba, ni muendelezo wa mikutano kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya sheria Zanzibar.



Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 

 

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top