WAHAMASISHAJI JAMII PEMBA, WAIBUA MENGI IKIWEMO KUKITHIRI KWA MAPENZI YA JINSIA MOJA.

Hassan Msellem
0

Wahamasishaji jamii Kisiwani Pemba wametakiwa kuendelea kuibua changamoto mbali mbali zinazowakabili wananchi ili ziweze kupatiwa ufumbuzi.

Akizungumza na wamahasishaji Jamii kutoka Wilaya ya Wete na Micheweni huko Ofisi za Pegao Chake Chake, mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari wanawake Tanzania TAMWA Kisiwani Pemba Bi. Fat-hiya Mussa Said, amesema miongoni mwa changamoto zinazopelekea wanawake wengi kushindwa kushiriki katika nafasi za uongozi ni pamoja ukosefu wa huduma bora za Afya.

 

Akiwasilisha mada muhamasishaji Jamii kutoka Wilaya Micheweni Bi. Asha Rashid Abdalla, amesema miongoni mwa changamoto walizoziibua katika Shehia ya Kinyasini Wizi wa mifugo, mazao pamoja na vitendo vya udhalilishaji.

 

Kwa upande wake muhamasishaji Jamii kutoka Wilaya ya Wete Husna Ali Said, amesema katika mkutano waliofanya na wananchi wa Shehia ya Limbani wamegundua idadi kubwa ya vijana wakiume wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja, jambo ambalo ni hatari kwa ustawi wa Jamii.

 

Nao washiriki wa mkutano huo wamesema wakati umefika kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuliangalia kina suala la Vijana wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja ili kuwachukulia hatua kali za kisheria.

 

Mradi huo wa kuwawezesha wanawake kushiriki katika nafasi mbali mbali za uongozi, unaendeshwa na Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania Tamwa Zanzibar, jumuiya ya mazingira na Utetezi wa kijinsia Pemba (PEGAO) pamoja Chama cha Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) na kufadhiliwa na Ubalozi wa Norway Tanzania.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top