WATATU MBARONI KWA TUHUMA ZA UHALIFU KENGEJA.

Hassan Msellem
0

Na, Hassan Msellem.

Watu watatu wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa Kusini Pemba kwa tuhuma za kumshambulia na vitu vyenye ncha kali Maulid Haroub Mpemba miaka 45, ambaye ni mfanya bishara wa miamala ya kifedha na wakala wa Banki ya watu wa Zanzibar PBZ mkaazi wa Makaange Kengeja Wilaya ya Mkoa wa Kusini Pemba.


Tukio hilo limetokea March 17.2023 majira ya saa 9 alfajiri huko Makaange Kengeja nyumbani kwa Ngudu Maulid Haroub Mpemba.

 

Akizungumza na Idawaonline.com Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba Kamishna msaidizi wa Polisi Abdalla Hussein Mussa alisema “Mnamo tarehe 17.03.2023 majira ya saa 9 alfajiri huko Makaange Shehia ya Kengeja Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba, watuhumiwa wasiojuilikana walivunja mlango wa nyumba ya bwana Maulid Haroub Mpemba mwenye umri wa miaka 45 Mkaazi wa Makaange kumshambulia na vitu vyenye ncha kali nab utu sehemu mbali mbali za kichwa chake chanzo cha tukio hilo bado kinachunguzwa kujua sababu ya kumjeruhi huyu muhanga baada ya tukio hilo watuhumiwa watatu walikamatwa kwa ajili ya mahojiano ambao ni Saleh Mohammed Abdalla maarufu Bambe miaka 33 mkaazi wa Mjiweni Kengeja, Salum Mohammed Seif maarufu Rumbwi miaka 46 mkaazi wa Tumbi Shehia ya Chumbageni na Mohammed Rashid Mohammed miaka 42 Mkaazi wa Mjiweni Kengeja”


Aidha Kamanda Abdalla, ametoa wito kwa wananchi kutii Sheria bila ya shuruti na kutokujichulia sheria mkononi.


Akikiri kupokelewa kwa Majeruhi huyo daktari dhamana wa hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani Rashid Saleh Hemed, alisema “Ni kweli tarehe 17.03.2023 majira ya saa 11:30 alfajiri tulimpokea ndugu Maulid Haroub Mpemba miaka 45 mkaazi wa Makaange Kengeja akiwa ameruhiwa sehemu mbali mbali kichwani majeruhi huyo alipatiwa matibabu lakini baadae tuliamua kumsafirisha kumpeleka hospitali ya Mnazi Mmoja kwa ajili ya uangalifu zaidi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top