Mbowe amjibu Sanga ataka wakutane 2025

0

 Kufuatia kauli ya mbunge wa Makambako, Deo Sanga ya kuitaka Chadema kutosimamisha mgombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe amesema watasimamisha wagombea ngazi zote kwa kuwa bado wanapambana na CCM.


Sanga (CCM) alitoa ombi hilo kwa Chadema bungeni jijini Dodoma juzi wakati akichangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi kwa mwaka wa Fedha 2023/23, huku akisema Mbowe hawezi kukataa maombi yake.

“Ombi langu kwa Mbowe, kwa sababu anataka kuwafanyia maendeleo Watanzania na mama ameshafanya kazi kubwa dunia inamwelewa, 2025 Mbowe tulia mwachie mama.

“2025 Mbowe shiriki na wabunge, shiriki na madiwani, nafasi ya urais mwachie mama,” alisema.

Akizungumza jana kwa simu na Mwananchi, Mbowe alisema Chadema haipo kwa ajili ya kumbeba Rais Samia.

"Sipendi sana kucomment in person kuhusu Sanga, lakini Chadema haipo kwa ajili ya kumbeba Rais Samia, atabebwa na chama chake (CCM). Tutapambama na Chadema kitakuwa na wagombea wa urais wazuri sina wasiwasi na hilo.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top