Mwandishi wa Habari ajutia Kuoa Wanawake wawili katika Maisha yake!

0

Mwanahabari  Maynard Manyowa kutoka nchini Kenya kupitia mtandao wa kijamii amefichua kuwa kosa lake kubwa maishani ni kuoa wake wawili.

Mwanamume huyo ambaye alijieleza kama mwanamume aliyekuwa na wake wengi, alikuwa akimjibu swali kutoka kwa wafuasi katika ukurasa wake kwenye Twitter ambaye alipendekeza kuwa ndoa ya mitala ndio bora zaidi

Alieleza kuwa anapinga ndoa ya wake wengi kwa sababu ya uzoefu wake binafsi na wake zake wawili, na akawataka wanaume waache mitala la sivyo hawatakuwa na amani katika maisha yao.

Kulingana na Maynard, anampenda mke wake wa kwanza na alimuoa mke wake wa pili ili kumwokoa kutoka kwa aibu ya kuwa mseja.

Hata hivyo, baada ya muda, alikaribia kumpoteza mke wake wa kwanza ambaye alimpenda sana kwa sababu alitaka kubaki na mke wake wa pili.

 "Kama mtu aliyekuwa katika ndoa ya mitala, nasema huu ni ushauri mbaya. Huwezi kuwa na amani kamwe katika maisha yako.

Nilikuwa na mke zaidi ya mmoja kwa sababu niliwahi kumpenda mwanamke mmoja tu.

 Na mwingine hakuwa Bibi wangu rasmi bali ni mtu ambaye sikutaka ateseke kwa sababu ya kutoolewa "Kosa kubwa zaidi kuwahi kutokea.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top