Jeshi la Polisi mkoani Mbeya alikiri kumshikilia Pwele

0

 Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, linamshikilia Musa Pwele(47) mkazi wa Jiji la Mbeya kwa tuhuma za kushiriki tendo la ndoa na mtoto wake wa kumzaa na kisha kumpa ujauzito.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP, Christina Musyani, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amedai mtuhumiwa amekamatwa Mei 5 mwaka  huu.

Amesema Pwele amekamatwa baada ya kumtishia binti yake wa kumzaa kuwa hatampatia huduma ikiwemo mahitaji ya shule na huduma nyinginezo na kutokana na shinikizo hilo alifanikiwa kumbaka mtoto wake.

"Upelelezi wa shauri hili unaendelea na mara baada ya kukamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani ili hatua stahiki zichukuliwe na kuwa fundisho kwa watu wengine," amesema Kamanda Christina.

Aidha Kamanda  Christina  ametoa wito  kwa wadau wa masuala ya kupinga ukatili wa kijinsia  kuendelea kutoa elimu  ili watu wenye tabia   hizo kuacha mara moja kwani vinasababisha  athari za kimwili na kisaikolojia kwa mtu mmoja na jamii.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top