JUMUIYA YA 'MDIPAO' YATOA MAFUNZO YA HAKI ZA BINADAMU KWA WANAWAKE NA WATU WA MAKUNDI MAALUMU 110, WILAYA YA MKOANI.

Hassan Msellem
0

Katibu Tawala Wilaya ya Mkoani Bi Miza Hassan Faki, amezitaka taasisi na jumuiya mbali mbali Kisiwani Pemba kuandaa miradi itakayowawezesha wanawake kuzitambua haki zao ikiwemo kujikomboa uchumi.

Ametoa kauli hiyo katika ufunguzi wa mafunzo ya siku ya kuwajengea uwezo wanawake na watu wa makundi maalumu katika masuala ya haki za binadamu huko Skuli ya Sekondari ya Pindua Mkanyageni Kisiwani Pemba, amesema tafiti zinaonesha bado wanawake wanakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo ukatili wa kijinsia, udhalilishaji pamoja na muhali.

 

Kwa upande wake mratibu wa Asasi za Kiraia Pemba Ashrak Hamad Ali, ameipongeza jumuiya ya wasaidizi wa Sheria Wilaya ya Mkoani (MDIPAO) kwa kuandaa miradi wa kutoa elimu ya haki za binadamu kwa wanawake kwani wanawake ndio wahanga wakuu katika vitendo vya uvunjifu wa haki za binadamu nchini.

 

Akifunga mafunzo hayo ya siku mbili afisa Sheria kutoka idara ya Katiba na Msaada wa Sheria Pemba Bakar Omar Ali, amesema kunzishwa kwa kampeni ya msaada wa Kisheria ya Mama Samia itasaidia kwa kiasi kikubwa kutoa elimu ya kisheria kwa akina mama.

 

Afisa Sheria kutoka idara ya Katiba na Msaada wa Sheria Pemba ndugu Bakar Omar Ali, ameipongeza Jumuiya ya Wasaidizi wa Sheria Wilaya ya Mkoani (MDIPAO) kwa kuandaa mradi utakaowawezesha wanawake kuzitambua haki zao ikiwemo kushiriki katika shughuli mbali mbali za kijamii.

 

Ametoa kauli hiyo wakati akifunga mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo wanawake na watu wa makundi maalumu katika masuala ya haki za binadamu huko Skuli ya Sekondari ya Pindua Mkanyageni Kisiwani Pemba, amesema tafiti zinaonesha kuwa wanawake na watu wenye ulemavu ndio wahanga wakuu wa vitendo vya uvunjifu wa haki za binadamu nchini ikiwemo kufanyiwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji.


Aidha amesema kunzishwa kwa kampeni ya msaada wa Kisheria ya Mama Samia itasaidia kwa kiasi kikubwa kutoa elimu ya kisheria kwa akina mama.

 

Akiwasilisha mada juu ya watu wenye mahitaji maalumu, Wakili wa Watoto Bi Siti Habib Mohammed, amesema miongoni mwa changamoto zinazowakabili watu wenye mahitaji maalumu ikiwemo watu wenye ulemavu ni pamona na kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji sambamba na kuitwa majina yasiyofaa.

Malik Mohammed Juma mkaazi wa Mkoani, ameiomba jumuiya hiyo kuendelea kupaza sauti za watu wa makundi maalumu ikiwemo watu wenye ulemavu na wasiojiweza ili waweze kupatiwa haki zao za msingi ikiwemo elimu, huduma za afya na lishe.


Naibu Mkurugenzi jumuiya za vijana umoja wa mataifa Mohammed Hassan Ali, amewataka washiriki hao kutokuwa na muhali na woga pindi wanapofanyiwa vitendo vya uvunjifu wa haki za binadamu ili wahusika wa vitendo hivyo waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.

Mkurugenzi wa MDIPAO Nassor Hakim Haji, Amewashukuru wafadhili wa mradi huo kwa msaada wake wa kuiunga mkono jumuiya hiyo Kwa lengo la kuwasaidia wanawake pamoja na watu wa makundi maalumu ili kuzitambua haki zao nchini.

Jumla ya wanawake na watu wa makundi maalum 110 kutoka Wilaya ya Mkoani wamepatiwa elimu ya haki za binadamu na haki nyengine kutoka Jumuiya ya wasaidizi wa Sheria Wilaya ya Mkoani (MDIPAO).




Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top