Mbaroni Kwa Kubaka na kukata sehemu za siri kisha kuzibanika Kwa Mganga!

0

Na:Henrick Idawa

Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza Limesema linawashikilia watu watatu akiwemo Mganga wa kienyeji kwa tuhuma za kumkata sehemu za siri mwanamke na kuzibanika ili kupata dawa ya uganga.

Akitoa taarifa hiyo kwa wandishi wa habari kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza Wilbroad Mutafungwa amesema walipokea taarifa za kifo cha mwanamke Esta  Lukoni jina maarufu kifebe (51) mkaazi wa kijiji cha Bugunangala aliyeuwa kwa kukabwa shingoni kisha kukatwa sehemu zake za siri na mwili wake kutelekezwa katika shamba la mihogo.

Amesema katika tukio hilo imeonesha marehemu aliingiliwa kimwili kabla ya mauji hayo ya kikatili.

“Kwani katika eneo la tukio ulipatikana mpira wa kiume uliotumika (condom),tukio hilo lilifanywa na watu ambao hawakufahamika” amesema mutafungwa

Kamanda Mutafungwa amesema jeshi la polisi baada ya kupata taarifa hiyo waliendelea na kufanya uchunguzi na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa.

“Watuhumiwa hao tuliwahoji wamekiri kuhusika na tukio hilo la ukatili baada ya kumbaka marehemu Esta Lukoni,kisha kumuua na kumkata sehemu yake ya siri”

Amesema katika watuhumiwa hao waliokamatwa yupo mganga wa kienyeji ambaye inadaiwa alipokea sehemu hizo za siri kisha kuzikausha kwa moto na kuzisaga kwa ajili ya matumizi ya uganga kwa imani potofu za kishirikina.

Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni “Masunga mabula (32),Ezekiel Charles (45) na Salome Rafael (32) na watuhumiwa hawa watafikishwa mahakamani mara uchunguzi utakapokuwa umekamilika”

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top