Hii ni Post ya tatu kwa msanii na mwanasiasa hapa nchini Prof Jay tangu aanze kuposti maendeleo ya afya yake baada ya kukaa kimya kwa zaidi ya mwaka mmoja wakati akiendelea kupata matibabu kushirikisha wafuasi wake kupitia social media,safari hii akija na oparesheni rudisha shavu kwa lugha nyingine unaweza kusema muda wa kula vizuri kurusisha mwili wa awali.
Katika Picha alizoshirikisha katika ukurasa wake wa Instagram Prof Jay ameandika 'Leo Nimeanza rasmi Oparation Rudisha Shavu , nikiwa na mdogo wangu wa damu @blackchatta hapa kwa @kazimotopork TABATA SEGEREA , Karibuni sana🙏🙏🙏'
Kupitia ukurasa wa chadema_in_blood walipost picha zake na Profesa Jay aka comments ujumbe huu 'Pamoja sana kamanda wangu najiandaa kuingia mzigoni kuungana nanyi kwenye mapambano✌️✌️✌️"