Mtoto adaiwa kumuua mama yake mdogo ili kuiba fedha za vicoba.

0

 Kijana wa miaka 15 (jina linahifadhiwa), mkazi wa Kijiji cha Ngareni, Kata ya Ngoyoni, wilayani Rombo, anashikiliwa na Jeshi la Polisi akidaiwa kumuua mama yake mdogo, Taudensia Massawe (62) kwa kumpasua kichwa akitumia jiwe wakati akikata majani ya ng'ombe.


Tukio hilo linadaiwa kutokea Aprili 24, mwaka huu baada ya kijana huyo kumwambia marehemu akamwonyeshe sehemu ya kukata majani ya ng'ombe na alipofika eneo aliloonyeshwa alimvizia wakati ameinama akikata majani na akampiga na jiwe lililompasua kichwa.

Kijana huyo anadaiwa kufanya mauaji hayo kwa lengo la kupora fedha za Vicoba ambazo mama huyo alikuwa mweka hazina na alikuwa na sanduku la fedha hizo.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top