Mwanamke afariki wakati maombi yakiendelea kanisani

0

 Mwanamke nchini Kenya alizirai na kupoteza maisha akiabudu katika kanisa moja la eneo bunge la Lang'ata katika kaunti ya Nairobi Jumapili - Mei 15, 2023.

Awali, mwanamke huyo alidhaniwa kuzirai tu na wahudumu wa kanisa wakaitwa kumsaidia, Lakini, hali yake ilivyozidi kuwa mbaya, ilikuwa wazi kuwa matibabu ya dharura yalikuwa yanahitajika.

Alikimbizwa katika Hospitali ya Mbagathi lakini madaktari wakabaini kuwa alikuwa amefariki hata kabla ya kufika katika hospitali hiyo.

Kamanda wa Polisi katika Kaunti ya Nairobi Adamson Bungei ameuthibitishia  umma kuwa uchunguzi unaendelea kumtambua marehemu na chanzo cha kifo chake.

 "Bado hatujabaini chanzo cha kifo chake Upasuaji wa mwili umefanywa ili kutusaidia katika uchunguzi wetu unaoendelea," Bungei alisema.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top