WAZIRI WA KAZI UGANDA AUAWA KWA KUPIGWA RISASI NA MLINZI WAKE.

Hassan Msellem
0

Waziri wa Kazi, Ajira na Uhusiano wa Viwanda Nchini Uganda Charles Okello, ameuawa  May 02, 2023 baada ya kupigwa risasi na mlizi wake ambapo Spika wa Bunge la Uganda Anitha Among amethibitisha kutokea kwa tukio hilo Bungeni.


Inaripotiwa kuwa Waziri Okello alikuwa anatoka Nyumbani kwenda kazini ambapo ghafla mlinzi wake alimpiga risasi kisha akaanza kupiga risasi juu huku akikimbiakimbia mtaani, majirani walisema walimsikia mlinzi huyo akisema hajalipwa mshahara kwa muda mrefu licha ya kufanya kazi kwa muda mrefu na Waziri huyo.

 

Kwa mujibu wa vyanzo vya taarifa hii vinasema mlinzi huyo baadaye aliingia saluni moja iliyopo jirani na nyumba ya Waziri huyo kisha akiwataka waliokuwa ndani kutoka nje na akajifungia na kujipiga risasi na kufariki pia.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

 


 

 




#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top