Kama huwa humalizi dozi uliyopewa na Daktari soma hii itakusaidia

0

 Ukaguzi wa dawa unaofanywa na mamlaka ya vifaa Tiba na Dawa(TMDA) umeelezwa kuwa na manufaa kwa watumiaji hivyo mamlaka hiyo imeiomba jamii kuiunga mkono.

Hayo yameelezwa Juni 06, 2023 na Mkaguzi wa Dawa kutoka Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba kanda ya Nyanda za juu Kusini Bi Grace Kapande wakati akitoa elimu ya matumizi ya dawa kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Iwawa wilayani Makete mkoani Njombe

Bi. Kapande ametumia nafasi hiyo kuieleza jamii kupitia wanafunzi hao kwamba kutokumaliza dozi ya dawa mgonjwa anayopewa na daktari inachangia usugu wa dawa

Tumezungumza na Gloria Haule, Magdalena Yona na Amani Elias wanafunzi wa shule hiyo ambao wamepatiwa elimu hiyo na kusema elimu hiyo wataifanyia kazi na kwenda kuifikisha kwa watu wengine

Mamlaka hiyo ya dawa na vifaa tiba ipo wilayani Makete mkoani Njombe ikiendelea kutoa elimu ya matumizi ya dawa kwa makundi mbalimbali kwa lengo la kuielemisha jamii ili iondokane na matumizi holela ya dawa.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top