Mchungaji Mwanza mbaroni kwa tuhuma ya kuwapotosha waumini

0

 JESHI la Polisi, mkoani Mwanza linamshikilia Herman Magigita (60) mkazi wa Kijiji cha Chema, Tarafa ya Kahunda, Wilaya ya Sengerema, mkoani Mwanza kwa tuhuma za kutoa mahubiri yenye kupotosha jamii.

Mtuhumiwa huyo ambaye ni mchungaji wa kanisa liitwalo NENO, alikamtwa baada ya kutoa mahubiri ya kupotosha waumini wake wasiende hospitali kupata matibabu pindi wanapougu, badala yake wawapeleke katika kanisa hilo kwa ajili ya maombezi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbroard Mutafungwa, ameeleza kuwa mtuhumiwa huyo alikamtwa baada ya jeshi hilo kupata taarifa za uwepo wa mchungaji huyo anayetoa mahubiri ya kupotosha na kufanya shughuli za kanisa bila kuwa na kibali cha usajili.
"Tulipata taarifa kuwa kuna mtu anatoa mahubiri ya kupotosha jamii, ambapo askari polisi walifika katika kanisa hilo na kufanikiwa kumkamata," alisema Kamanda Mutafungwa.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

JIUNGE NA IDAWA MEDIA SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Telegram na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka IDAWA TV Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube & Jiunge WhatsApp 

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top